BREAKING NEWS
Showing posts with label Aunty Ezekiel. Show all posts
Showing posts with label Aunty Ezekiel. Show all posts

Tuesday, 5 July 2016

Moses Iyobo Amtaka Mama Cookie Ajichore Tattoo Kama Shilole

Dansa kutoka Wasafi Classic Baby (WCB), Moses Iyobo ‘Moze’ ambaye ni mzazi mwenza wa staa wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel Grayson, amemwambia mpenzi wake huyo kuwa na yeye ajichore ‘tatuu’ ya jina lake kama ilivyokuwa kwa msanii Zuwena Mohammed ‘Shilole’ kwa Naftal Mlawa ‘Nuh Mziwanda’ kabla ya kumwagana.

Moze alimwambia hayo Aunt baada ya mwanadada huyo kujichora mkononi kwa kalamu maneno yaliyosomeka; ‘Aunt wa Mose Iyobo’ ambapo jamaa huyo alimsisitizia kuwa kama kweli anamaanisha hivyo, basi ajichore kama Shilole alivyofanya kwa Nuh.

“Kama mama Cookie (mtoto wao) anataka kujilipua, ajichore kama Shilole alivyofanya kwa Nuh maana alivyojichora kwa kalamu, hata akioga, inatoka,” alifunguka Moses.

Friday, 1 July 2016

Wema Sepetu Afungukia Ugomvi Wake na Aunt Ezekiel

STAA wa filamu Bongo, Wema Sepetu amefungukia ugomvi ambao hutokea mara kwa mara na shosti wake ambaye pia ni muigizaji, Aunt Ezekiel usiingiliwe na mtu kwani wanapogombana tofauti zao wanazimaliza wenyewe na si mtu mwingine yeyote.

Akizungumza na Amani Wema alisema kuwa, yeye na Aunt ni watu waliopo karibu sana na wanaopendana hivyo inapotokea wanagombana huwa ni kitu kidogo kwao kwani huyamaliza na maisha yanaendelea kama kawaida.

“Jamani nyinyi mtuache tu, tunatibuana na Aunt, tunajuana vizuri sana ugomvi wetu ni wa mara kwa mara lakini tunamalizana wenyewe kwa sababu ukweli ni kwamba hatuwezi kukaa mbalimbali kwa muda mrefu kutokana na kupendana,” alisema Wema.

Chanzo:GPL
 
Copyright © 2014 Kali Za Wana. Designed by OddThemes