BREAKING NEWS
Showing posts with label Shaa. Show all posts
Showing posts with label Shaa. Show all posts

Monday, 18 July 2016

Mwaimbaji Shaa Hayupo Tena Katika Lebo Hiyo Inayomilikiwa na Master Jay

Malikia wa uswazi kama mwenyewe anavyopenda kujiita Shaa ameweka wazi zile tetesi zilizokuwa zimezagaa kwamba ameondoka Mj Record na kesema ni kweli hayupo chini ya lebo hiyo lakini haimaanishi kwa hafanyi kazi na studio za Mj .

Hata hivyo Shaa amesema ameanzisha kampuni yake inayoitwa SK ambayo ni matokeo ya kazi za sugua gaga,toba na nyingine ambazo zilirudisha gharama za Mj na kumuwezesha kufungua kampuni hake hiyo binafsi ambayo anatarajia kusajili wasanii hata wa tano ila kwa sasa yupo yeye peke yake.

Hata hivyo Shaa ameachia wimbo wake mpya unaoitwa Sawa kupitia kampuni yake hiyo ila unaambiwa Shaa hayupo taari kuyazungumzia mahusiano yake kama ailivyo mpenzi wake Master J ambaye akiulizwa na huwa anajibu lakini kwa Shaa nitofauti kabisaa

Wednesday, 15 June 2016

Master J na Shaa kufunga ndoa

Mtayarishaji mkongwe wa muziki nchini, Joachim Kimaryo ‘Master Jay’, ameweka wazi mpango wake wa kufunga ndoa na mpenzi wake wa muda mrefu, Sara Kaisi ‘Shaa’.
Shaa na Master Jay
Master J amesema Shaa atakuwa mke bora kwake kwani tayari ameshaishi naye kwa miaka 10 bila matatizo yoyote.
“Miaka 10 niliyoishi naye nimemwelewa vizuri, anastahili kabisa kuitwa mke wa Master J hapa nafanya taratibu za kumuoa ili tuishi maisha ya mke na mume,” Master J aliliambia gazeti la Mtanzania.
Mtayarishaji huyo wa muziki alisema kwamba anampenda Shaa kwa sababu ni msichana anayejielewa, licha ya kuwa msanii hasahau jamii inayomzunguka huku akijituma sana katika kazi zake zote kwa ujumla
 
Copyright © 2014 Kali Za Wana. Designed by OddThemes