BREAKING NEWS
Showing posts with label Michezo. Show all posts
Showing posts with label Michezo. Show all posts

Friday, 29 July 2016

Usajili wa Paul Pogba Manchester United Kukamilika Masaa 48 Yajayo.


post-feature-image
Klabu ya Manchester United inatarajiwa kumsaini kiungo wa Juventus Paul Pogba ndani ya masaa 48 yajayo baada ya kukubali kulipa ada ya wakala wake.
Taarifa za ndani ya klabu hiyo zimedai kuwa tayari zimeshakubaliana na Juventus kwa ada ya uhamisho wa mchezaji huyo ambaye anatarajiwa kufanya vipimo vya afya yake muda wowote huko nchini Marekani alipokuwa kwa kwenye mapumziko yake ya kujiandaa na msimu mpya.

Pogba anatarajiwa kuweka rekodi ya kuwa ndiye mchezaji ghali zaidi kuuzwa kweye tasnia ya soka huku ikikadiriwa kuwa United wamekubali kulipa kiasi cha zaidi ya paundi milioni 100 ili kuipata saini ya mchezaji huo mwenye miaka 23 anayewaniwa na timu nyingine ya Madrid.

Aidha imedaiwa kuwa wakala wa mchezaji huyo, Mino Raiola anadaiwa ndiye chanzo cha kuchelewesha dili la usajili wa mchezaji huyo kwa kutaka kulipwa kitita cha paundi milioni 25 nje ya pesa za usajili wa mchezaji huyo.

Pogba anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka mitano wa kuichezea timu hiyo na kupokea mshahara wa paundi 290,000 kwa wiki na atakuwa ni mchezaji wa nne kusajiliwa chini ya kocha mpya, Jose Mourinho akiwa mpaka sasa kasha msajili Eric Bailly, Henrikh Mkhitaryan na Zlatan Ibrahimovic.

Monday, 18 July 2016

Baada ya Kufunga Goli Kwenye Mchezo wa Europa League Samatta Afunguka

Mtanzania Mbwana Samatta aliweka rekodi ya kufunga katika michuano ya Europa League baada ya timu yake ya Genk kuibuka na ushindi wa magoli 2-0 mbele ya Budućnost ya Montenegro.

Clouds FM kupitia kipindi chake cha michezo cha Sports Extra kilifanya mahojiano maalu na Samatta kutaka kujua mambo mbalimbali. Mtandao huu ukaona haitakuwa vibaya kama utakuletea kile alichokisema nyota huyo hasa kama ulikosa kusikiliza show ya Sports Extra.

sportsextra: Mbwana Samatta unajisikiaje kuwa Mtanzania wa kwanza kufunga goli katika michuano ya Europa League?

Samatta: Nimejisikia vizuri kwasababu ndiyo kitu ambacho kila siku nakipigania kuweza kufanikiwa, mshambuliaji unaweza kufunga magoli, nimejisikia vizuri na inanipa morali zaidi ya kuendelea kujituma.

sportsextra: Ulianza katika kikosi cha kwanza mbele ya Nikola Karelis mshambuliaji wa kutumainiwa wa Genk, hii inamaanisha kuwa mwalimu Peter Maes anakuamini sana kuliko mshambuliaji huyo anayehusishwa na kujiunga na klabu ya Nottingham Forest ya nchini England?

Samatta: Nafikiri sasahivi mwalimu ananiamini na anapenda kunitumia, ni kitu ambacho kwakweli ni kizuri kwangu mwenyewe binafsi lakini pia nafikiri yeye kwake anaona namsaada mkubwa kwenye timu yake nikiwa naanza kwenye kikosi cha kwanza. Nafikiri ni jambo la kusubiri muda utakapofika kilakitu kitakuwa wazi lakini kwa sasahivi nafikiri mwalimu anapenda kunitumia zaidi.

sportsextra: Watu wengi walikuwa wanajaribu kujiuliza kuwa Mbwana yupo wapi wakati wa likizo yako baada ya kusimama kwa Ligi Kuu ya soka nchini Ubelgiji. Watu wanataka kujua ulikuwa wapi Mbwana wakati wa mapumziko?

Samatta: Likizo nilikuwa Tanzania japo likizo ilikuwa fupi lakini nilikuwa nyumbani nimepumzika ilikuwa ni kipindi cha mwezi wa Ramadhani kwahiyo nilikuwa kwenye mfungo. Ilikuwa haina sababu ya kuonekana kwasababu ilikuwa ni kipindi cha mapumziko.

Ukifata program ya mazoezi kutoka kwenye timu, ilikuwa ni muda wa kupumzika kwa wiki moja halafu wiki nyingine unatakiwa ufanye mazoezi wewe mwenyewe binafsi. Lakini kwa bahati mbaya mimi sikupata muda wa kupumzika kwasababu wakati likizo inaanza mimi nilitakiwa nijiunge na timu ya taifa kwa ajili ya mechi dhidi ya Misri na baada ya hapo niliendelea na program ambayo nilipewa mimi binafsi.

Mchezaji anapopewa likizo anatakiwa apumzike kabisa kwasababu ni kipindi ambacho mwili wake unatakiwa ujirudi na kutengeneza nguvu mpya. Haina maana kwamba ukipewa likizo basi ujifue na kujiweka nondo hapana, muda wa mapumziko ni kipindi ambacho anatakiwa apumzike kama amepewa program basi afanye lakini asijichoshe.

sportsextra: Mbwana nafasi ya timu yako ya Genk sasa unaionaje katika michuano ya Europa League baada ya jana kupata ushindi mbele ya klabu ya Budućnost?

Samatta: Nafikiri bado tunakibarua kwasababu ni mechi ya kwanza na tumeshinda kwa goli 2-0, mpinzani sasahivi kichwani kwake anajua kwamba amefungwa goli mbili na anahitaji kurudisha na kupata ushindi akiwa nyumbani, kwahiyo kibarua bado kipo siwezi kusema moja kwa moja kwamba tutakata tiketi ya kucheza kwenye makundi lakini nafikiri tuna timu nzuri na tunaweza kufika huko kwa hiyo kila kitu ni wakati.

sportsextra: Asante sana Mbwana Samatta.

Haya Ndio Majibu Ya Vipimo VYa Demba Ba Baada Ya Kuvunjika Mguu

BA
Picha za X-ray imeonyesha, mguu wa kushoto wa mshambuliaji kutoka nchini Senegal, Demba Ba amevunjika mfupa wa ugoko na huenda ikamchukua muda kupona jeraha hilo.
Ba, alikimbizwa hospitali baada ya kupatwa na maswahibu hayo akiwa katika mchezo wa ligi kuu ya soka nchini China, ambapo klabu yake ya Shanghai Shenhua ilikua ikipapatuana Shanghai SIPG ambao mwishowe walikubali kupoteza kwa kufungwa mabao mawili kwa moja.
Wakati Ba akipatwa na majeraha ya kuvunjika mguu, Shanghai Shenhua walikua nyuma kwa bao moja kwa sifuri.
 
Picha ya X-Ray inayoonyesha jeraha la Demba Ba
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 31, alipofikisha hospitali lipatiwa matibabu ya awali na kupewa dawa za usingizi ambazo zilimchukua muda wa saa nne kabla ya kuamka.
Daktari anayemtibu Ba, alisema kwamba swali la kwanza alilouliza mshambuliaji huyo ambaye aliwahi kucheza soka katika ligi ya nchini England lilikuwa ni kutaka kufahamu matokoe ya mchezo aliouacha ukiendelea.
“Tumeshinda mchezo wetu?” hivyo ndivyo alivyoniuliza, alisema daktari huyo
 
Naibu meya wa jiji wa Shanghai Zhao Wen alipomtembelea Ba hospitali
Mwenyekiti wa klabu ya Shanghai Shenhua, Wu Xiaohui alifika hospitalini hapo kumjulia hali Ba, baada ya kuzinduka kutoka usingizi na amemtakia kila la kheri katika kipindi hiki cha kujiuguza jeraha lake.
Katika hatua nyingine mchezaji aliyemvunja Ba, Sun Xiang naye alifika hospatali kumjulia hali, pamoja na naibu meya wa jiji wa Shanghai Zhao Wen.

Friday, 1 July 2016

Ureno Yachapa Mtu Robo Fainali ya Euro

ureno
ureno
Ureno imetinga hatua ya nusu fainali katika michuano ya Euro inayoendelea nchini Ufaransa na kuwa nchi ya kwanza kufuzu katika hatua hiyo baada ya kuwafunga Poland kwa mikwaju ya penalti 5-3.
Dakika 120 zilishuhudia mchezo huo ukiisha kwa suluhu ya goli 1-1.Robert Lewandowski aliiandikia goli Poland mapema kipindi cha kwanza katika dakika ya tatu ya mchezo kabla ya Renato Sanches kuisawazishia timu yake ya Ureno.
Ricardo Quaresma alikuwa shujaa kwa timu yake baada ya kupiga penalti ya mwisho iliyoivusha katika hatua nyingine huku kiungo wa Jakub Blaszczykowski akikosa mkwaju wa penalti kwa upande wa Poland.
Ureno itakutana katika hatua ya nusu fainali na mshindi wa mchezo kati ya Wales na Ubelgiji.

Thursday, 30 June 2016

Rasmi: Zlatan Ibrahimovic ataja timu atakayoichezea msimu ujao

Aliyekuwa mchezaji wa timu ya PSG, Zlatan Ibrahimovic ametangaza rasmi kuwa ataichezea timu ya Manchester United kwa msimu ujao utakaoanza Agosti 13 mwaka huu.
Kadabra
Ibrahimovic ambaye alikuwa akiwaniwa na United kwa muda mrefu tangu alipomaliza mkataba wake na PSG sasa atakuwa ni mchezaji wa pili kusajiliwa na Jose Mourinho baada ya beki wa Ivory Coast, Eric Bertrand Bailly kutoka Villarreal kusajiliwa mapema mwezi huu.
Aidha Ibrahimovic (34) atasajiliwa kama mchezaji huru na Manchester United huku akitarajiwa kusaini mkataba wa mwaka mmoja kuichezea timu hiyo.
 
Copyright © 2014 Kali Za Wana. Designed by OddThemes