BREAKING NEWS
Showing posts with label Udaku. Show all posts
Showing posts with label Udaku. Show all posts

Tuesday, 19 July 2016

Mtoto wangu wa kike ataitwa Karma – Wema


wema

Malkia wa filamu Wema Sepetu bado hajakata tamaa kuhusu kupata mtoto licha ya kukatishwa tamaa na baadhi ya watu katika mitandao ya kijamii kutokana na uzazi wake kuwa mgumu.

Muigizaji huyo ambaye alianzisha mfumo wa APP na SMS ambao unatoa taarifa zake mbalimbali kwa mashabiki juu ya maisha yake, tayari umeanza kutoa taarifa mbalimbali kuhusu maisha yake.
Kupitia mfumo huo, Wema amesema angependa mwanae wakiume ampatie jina la Karma.
“Mtoto wangu wa kiume ataitwa Karma,” alisema Wema. “Bado sijafikiria jina nitakalo mpa mtoto wangu wa kiume japo namtaka sana mtoto wa kwanza awe wa kiume, Mungu anajua,” alisema Wema.
Pia kupitia system hiyo, Wema amewashukuru mastaa wenzake wa filamu ambao walimsupport katika show yake ya ‘The Black Tie’.

Jose Chameleone Katika Bifu Zito na Diamond Platnumz....? Ukweli Halisi Huu Hapa

post-feature-image


Msanii mkongwe wa muziki kutoka nchini Uganda, Jose Chameleone amefunguka kwa kusema kuwa hana tatizo na hit maker wa wimbo ‘Kidogo’, Diamond Platnumz.

Mitandao ya kijamii ilidai wawili hao hawakuwa sawa kwa muda mrefu kutokana na madai ya kuwa Jose Chameleone kumdengulia Diamond baada ya kuombwa kolabo, lakini hakuna aliyewai kuzungumzia tetesi hizo.

Jumanne hii Jose amesema hakuwai kuwa na tatizo na Diamond kama baadhi ya watu wanavyozungumza.

“I know how much hard work it takes to build a name and how we are all relevant to flying Africa Music to the world. I can see people trying to build beef lines between me and Diamond Platnumz all these years,” aliandika Jose kupitia instagrm.

Aliongeza, “All I can say is go higher my brother the sky ain’t the limit.Stay strong and God bless you more,”

Baada ya kusema hivyo, mashabiki wa Diamond pamoja na wadau mbalimbali wa muziki katika mitandao ya wamempongeza Jose Chameleone.

Sunday, 10 July 2016

Kiki za Mastaa Zilizotingisha, Shilole, Vanessa Mdee, Ray Kigosi, Rubby, Aslay….

KIKI siyo kitu kigeni kabisa kwa wasanii ulimwenguni. Kutafuta jambo la kushtua na kuwafanya mashabiki wamzungumzie msanii husika kwa muda mrefu zaidi akiwa na lengo la kuachia kazi yake.


Lakini kwa baadhi ya wasanii wetu hapa Bongo hujiingiza kwenye skendo wakidhani ni kiki. Kwa kawaida kiki ni nzuri ili kumsaidia msanii kujipaisha na kuchomoa kazi yake, lakini si kwa kujiharibia kwa kashfa mbaya ambazo mwisho wake kufutika inakuwa shida.

Yes! Hapa Bongo wapo mastaa wengi ambao wametingisha kwa kiki huku wengine wakijaribujaribu. Polisi wa Swaggaz anakudondoshea kiki za mastaa zilizotingisha zaidi tangu kuanza kwa mwaka huu.

RUBY, ASLAY

Kila mtu aliongea lake ilipovuma kuwa Ruby anatoka na Aslay ambaye kiumri ni mdogo kwake. Hii ilitokea Juni 13, mwaka huu mara baada ya Ruby kuanza kutupia picha za Aslay kwa fujo kwenye ukurasa wake wa Instagram na kuandika meneno yanayoashiria kuna mahaba mazito kati yao.

Aslay yeye alimjibu Ruby kwa jumbe tamu za mahaba na kuzidi kuwachanganya mashabiki huku wengi wakitamani kuona kama penzi hilo jipya mjini litakuwa na uzito wa kuipiku kapo ya Harmonize na Wolper iliyokuwa inatamba kipindi hicho.

Wakati watu wengi wanazidi kumiminika na kuifuatilia kapo hii ndipo Yamoto Band wakaachia ngoma yao mpya inayoitwa Suu, waliyomshirikisha Ruby.

Ikasanuka kumbe ilikuwa kiki tu. Hilo lilithibitishwa hata na meneja wao Said Fella ‘Mkubwa Fella’ a.k.a Mheshimiwa Diwani.

LINEX

“Ahsante Mungu, kuna maamuzi hayahitaji matangazo, silence speaks  volumes,” aliandika Linex kwenye ukurasa wake wa Instagram mara baada ya kutupia picha akiwa kwenye mikao tofauti na mrembo aliyedai kuwa amemuoa.

Linex alizidi kupokea pongezi kutoka kwa mashabiki waliovutiwa na tukio la yeye kufunga ndoa, uamuzi ambao ni nadra mno kwa wasanii wa Bongo Fleva.

Hali ilikuwa tofauti mara baada ya kutumia picha zilezile za harusi kutengeneza kava la ngoma yake mpya iitwayo Kwa Hela, aliyoachia mwanzoni mwa mwaka huu.

Kwa tukio hilo, Linex alijikuta akipokea matusi kutoka kwa mashabiki kwa kosa la kuchezea hisia zao lakini mbali na kadhia hiyo lengo lake la kutumia Kiki lilifanikiwa, aliapoachia ngoma yake ikapenya.

RAY KIGOSI

Vincent Kigosi ‘Ray’ alifanikiwa kuwakamata mashabiki wake kwa kutengeneza kiki yenye ‘akili’ sana. Yeye aliibuka na maelezo kuwa weupe wake ni kwa sababu anatumia maji mengi na kushiriki mazoezi.

Ray alisema hayo wakati akihojiwa na kituo kimoja cha runinga jijini Dar es Saalam. Hakuna kiki inayofikia hii tangu mwaka huu umeanza. Katika mitandano ya kijamii watu mbalimbali walipiga picha wakiwa wanakunywa wakidai wanataka kuwa weupe kama Ray!

Ile kushangaashangaa, Ray akaachia Filamu ya Tajiri Mfupi ambayo ilifanya vizuri sokoni. Pamoja na kiki hiyo, Tajiri Mfupi ni kati ya sinema bora za Kibongo zilizotoka mwaka huu.

VANESSA MDEE

“Nikupe Kiki ujulikane au siyo? Kila siku twanyamaza ndiyo mtugaragaze. Mimi siyo wale uliowazoea,” aliandika Vanessa Mdee kwenye instagram akimshambulia Shilole.

Shilole hakukaa kimya naye kupitia ukurasa wake wa Instagram aliandika: “Veepe jipange sana, mwenzio Igunga niliaga, sijaletwa kwa kubebwa kwenye lori, nimekuja na mbio za mwenge. We si wa magorofani na kiingereza chako cha kuunga mi ndo mtoto wa mbwa, sasa ole wako tukutane utanyooka.”

Watu wakahamishia mawazo yao kwao, kutahamaki kumbe walikuwa wanaandaa shoo Club Bilicanas, Dar. Shoo ilikuwa poa kutokana na kiki hiyo.

NEDY MUSIC

Baada ya Shilole kumwagana na Nuh Mziwanda watu walikuwa wanatamani kufahamu ni nani ataziba pengo hilo. Ghafla kijana mdogo Nedy Music akaanza kuhisiwa kutoka kimapenzi na mwanadada huyo.

Sababu kubwa iliyofanya watu waanze kuhisi kuwa kuna penzi kati yao ni picha walizokuwa wanatupia kwenye Instagram zikiambatana na maneno ya mapenzi.

Hakuna aliyemjua Nedy Music kabla ya kuwa na Shilole lakini alipata umaarufu mara baada ya kiki hiyo ya kumrithi Nuh Mziwanda, hata  alipoachia ngoma yake Usiende Mbali chini ya Ommy Dimpoz kupitia lebo ya PKP alichomoka kirahisi tu.

Na hapo ndipo ikajulikana kuwa hakukuwa na mapenzi kati yao bali ilikuwa kiki ya kutafuta mashabiki kwenye muziki huu wenye ushindani. Kwa hilo alifanikiwa.

Diamond na Zari Waweka Video yao Wakiwa Nusu Utupu Baada ya Kumaliza Mechi Sita Kwa Sita..Tazama Hapa

Instagram inazidi kuwa sehemu ya mastaa kujitamba na mambo tofauti wanayofanya kwenye maisha yao kama vitu vya kifahari, mali zao na watoto wakali wanaotoka nai,

HAMISA Mobeto Afunguka Tuhuma za Kutoka na Diamond Kimapenzi Zilizoenea Mtandaoni


Hamisa Amefunguka haya baada ya tetesi kuzagaa mtandaoni kuwa yeye ndio chombo kipya cha Diamond baaada ya kuonesha ukaribu zaidi na familia ya Dai:

"Eti Mdau anauliza kama ilikuwa kazi mbona hukupiga picha na Madam Zari?
Chaaaa!!! From @hamisamobetto - Binadaamu banaa.......
Now days U cant work with anyone wala kua close na yoyote just because unaogopa maneno yatakayo zuka after hiyo shughuli ...
@kendrah_michael @_esmaplatnumz
A birthday to remember 2016
#MamasBigDay ....... Na nshaanza kupokea emails za kazi ety...haya kama unataka upendezeshwe na Hamisa mobeto ung'are sherehe yako iwee ya kuvutia kindly contact me kwa email ya apo kwenye Bio
#HapaKaziTu ...Cc the boss @diamondplatnumz"

Tuesday, 5 July 2016

Moses Iyobo Amtaka Mama Cookie Ajichore Tattoo Kama Shilole

Dansa kutoka Wasafi Classic Baby (WCB), Moses Iyobo ‘Moze’ ambaye ni mzazi mwenza wa staa wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel Grayson, amemwambia mpenzi wake huyo kuwa na yeye ajichore ‘tatuu’ ya jina lake kama ilivyokuwa kwa msanii Zuwena Mohammed ‘Shilole’ kwa Naftal Mlawa ‘Nuh Mziwanda’ kabla ya kumwagana.

Moze alimwambia hayo Aunt baada ya mwanadada huyo kujichora mkononi kwa kalamu maneno yaliyosomeka; ‘Aunt wa Mose Iyobo’ ambapo jamaa huyo alimsisitizia kuwa kama kweli anamaanisha hivyo, basi ajichore kama Shilole alivyofanya kwa Nuh.

“Kama mama Cookie (mtoto wao) anataka kujilipua, ajichore kama Shilole alivyofanya kwa Nuh maana alivyojichora kwa kalamu, hata akioga, inatoka,” alifunguka Moses.

Monday, 4 July 2016

​Picha: Ommy Dimpoz, Wayne Rooney Wakila Bata Ibiza, Hispania

Kama kuna sehemu inayotembelewa zaidi duniani na watu ambao hawana kabisa stress ya kitu kinachoitwa ‘Pesa’ basi Ibiza, Hispania inaongoza.

Ibiza ni kisiwa cha raha, burudani, starehe na bata la kila aina. Ni sehemu ambayo nyota wa Manchester United na England, Wayne Rooney na familia yake wanapumzika kwa sasa baada ya timu yake ya taifa kutolewa kwenye Euro 2016.
Ommy Dimpoz ni miongoni mwa watu wanaofurahia hewa ya Ibiza kwa sasa.

Hitmaker huyo yupo kisiwani humo katika kile kinachoweza kuwa ni ‘vekesheni’ yake ya aghali zaidi kuwahi kuifanya.

Anamfanya kila mtu aone wivu kwa maisha na raha anayopitia sasa. Kucruise kwenye speed bot na kuchezea maji ya bahari ya Mediterranean.

Staa huyo amepost video akiwa kwenye boti na watu wengine wawili, msichana , Milly na nahodha wa kizungu aliye kifua wazi. Hakika Ommy katisha.

Barakah Da Prince adai hajawahi kuupenda muziki wa Young Killer

Msanii wa muziki, Barakah Da Prince, amefunguka na kusema kuwa yeye si shabiki na wala hapendi muziki anaoufanya rapa na mzaliwa mwenzie wa Mwanza Young Killer Msodoki.Barakah Da Prince
Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo ‘Siwezi’ ameiambia Times Fm, kuwa hapendi muziki wala hajawahi kupenda kazi yoyote ya Msodoki.
“Sijawahi kupenda muziki anaoufanya Killer,” alisema Barakah. “Mi sio shabiki yake kabisa, najua ndio anatokea home na nini lakini sipendi muziki wake,”
Katika hatua nyingine amesema rapa anayemkubali zaidi ni Young Dee kwa kuwa anauwezo wa kubadilika kulingana na Mazingira.

Bongo5.com

Mo Music Adata Kwenye Penzi Na Baby J

mo musicMKALI wa Bongo Fleva, Moshi Katemi ‘Mo Music’ anadaiwa kunasa ‘kimalovee’ na msanii mwenzake, Jamila Abdallah ‘Baby J’ ambaye muda mwingi makazi yake ni Zanzibar, lakini mara kwa mara wamekuwa wakionekana kujiachia maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar.
Kwa mujibu wa chanzo chetu kilichopo karibu na wasanii hao kilieleza kuwa, hiyo ndiyo kapo mpya ya mjini licha ya kuwa, hawajaamua kuweka wazi uhusiano wao kwa mashabiki lakini si siri tena sababu hata wasanii wenzao wengi wanafahamu.
Jamila Abdallah ‘Baby J’ 
Jamila Abdallah ‘Baby J’
Baada ya kuupata ubuyu huo, mtandao wa Global Publishers ilimvutia waya Baby J ambaye aliruka vikali na kudai ni mtu wake wa karibu tu, upande wa pili Mo Music alipotafutwa alianza kwa kuangua kicheko na kusema kuwa;
“Kweli mjini mtu hakunyimi umbeya sijui mmeyapataje haya, sioni cha ajabu hapo ila muda ukiwadia nitaweka wazi kila kitu.”

Wastara Anunua Mjengo Wa Mil 180


wastara nyumba (5)Wastara akipiga picha na wenyeji wa eneo hilo.
STORI: HAMIDA HASSAN WIKIENDA
Dar es Salaam: Huku kukiwa na madai mazito ya kumchuna aliyekuwa mumewe ambaye ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa na Mbunge wa Jimbo la Donge, Zanzibar, Sadifa Khamis Juma, staa wa sinema za Kibongo, Wastara sasa anaripotiwa kununua mjengo wenye gharama ya Sh. milioni 180 za Kitanzania, Wikienda limechimba.
wastara nyumba (3)Mjengo alioununua Wastara.
Pamoja na misukosuko yake na Sadifa, ubuyu kutoka kwa mtu wa karibu wa Wastara unanyetisha kuwa Wastara kwa sasa mambo yake ‘supa siyo dizeli’ kwani anaonekana mshiko umemtembelea na kununua nyumba hiyo iliyopo Gongo la Mboto, Dar.
wastara nyumba (4)
“Jamani nawapa ishu lakini msinitaje, lakini ukweli ni kwamba Wastara amenunua nyumba maeneo ya Gongo la Mboto.
“Wapo wanaosema eti mbwembwe zote anazifanya na fedha alizomchuna Sadifa lakini pia wapo wanaosema kuwa nyumba hiyo amepangishiwa na aliyekuwa mpenzi wake, Bond Bin Sanan kwani maeneo aliyonunua nyumba hiyo ndiyo anayokaa Bond,” alifunguka ‘kikulacho’ huyo.
wastara nyumba (2)
Sosi huyo aliendelea kunyetisha kuwa, pamoja na kwamba Wastara kwa sasa yupo nchini Msumbiji kibiashara (anafanya biashara ya nguo) lakini nyumba hiyo wanakaa watoto wake.
Baada ya habari hiyo kutua kwenye meza ya Wikienda, mwanahabari wetu alimtafuta Wastara kwa njia ya simu baada ya kuhakikishiwa kuwa hayupo Bongo, alipopatikana alikiri kununua nyumba kwa Sh. milioni 180.
wastara nyumba (1)
Katika mahojiano ya Wikienda na Wastara, mambo yalikuwa hivi;
Wikienda: Wastara kuna madai kuwa umepangishiwa nyumba na Bond kwa sababu mmerudiana ingawa wapo wanaosema umeinunua, je, hilo likoje?
Wastara: Unajua watu wanapenda kunizushia lakini mimi sipendi. Huyo Bond sijarudiana naye bali ninaongea naye kwa sababu ya kazi (uigizaji). Kuhusu nyumba nimenunua mwenyewe.
Wikienda: Kuna madai mengine kuwa fedha ulizonunulia nyumba ulimchuna mbunge (Sadifa), wewe unasemaje?
Wastara: Kwanza mimi sikuona fedha ya kumchuna huyo mbunge na hakuna fedha aliyonipa. Mimi ni mfanyabiashara, biashara zangu za madini, nguo na urembo ndizo zinaniingizia fedha. Ifahamike kuwa nilianza kufanya biashara tangu kitambo.
Wikienda: Je, ni kweli umeuza nyumba yako ya Tabata? Au ni kwa sababu inatakiwa ibomolewe hivyo umeisusa?
Wastara: Sijaiuza, naikarabati, Mungu akipenda nitawaweka watoto yatima kwani ndiyo mipango yangu ya siku nyingi.
Sadifa alipotafutwa kwa njia simu ili kusikia kauli yake, hakuweza kupatikana hewani jitihada zinaendelea.

Maiti ya Mtoto Yapiga Kelele Wakati Ikioshwa..!!

  maiti ya mtoto (3)Waombolezaji wakienda kuzika mwili wa marehemu, Rahim Fikiri.
STORI: DUSTAN SHEKIDELE, WIKIENDA
Morogoro: Haijawahi kutokea! Kwenye Kijiji cha Melela, Mlandizi wilayani Mvomero mkoani hapa, kumegubikwa na simanzi nzito kufuatia maiti ya mtoto, Rahim Fikiri (2), kukumbwa na mauzauza kibao yakiwemo kupiga kelele wakati wa kuoshwa, mwili kutoka jasho kali na kuliwa macho na masikio.
maiti ya mtoto (2)
MASHEHE WALAZIMIKA
Tukio hilo la kusikitisha lilijiri wiki iliyopita nyumbani kwa wazazi wa mtoto huyo kijijini Melela, Mlandizi hivyo kuwalazimu mashehe kuingilia kati na kushusha dua nzito iliyoondosha mauzauza hayo.
Kufuatia tukio hilo, baadhi ya wananchi wa kijiji hicho walimtonya mwanahabari wetu aliyefika katika kijiji hicho kilichopo umbali wa kilomita 40 kutoka mjini Morogoro ambapo alikutana na msafara wa kuelekea makaburini kwa ajili ya mazishi.
maiti ya mtoto (4) 
Bibi wa marehemu, Elizabeth Josefu.
BIBI ALIYESHUHUDIA
Akizungumzia tukio hilo, bibi wa marehemu aliyeshuhudia mauzauza hayo, Elizabeth Josefu alikuwa na haya ya kusema:
“Nilipigiwa simu nikaelezwa kwamba mjukuu wangu amelazwa Kituo cha Afya cha Melela. Nilipofika nilielezwa kuwa alipopimwa, alikutwa ana upungufu wa damu.
maiti ya mtoto (1)“Aliongezewa damu na baba yake lakini hali yake ilizidi kuwa mbaya hivyo tulipewa rufaa ya kumpeleka Hospitali ya Mkoa. Tulipofika huko tuliambiwa ana degedege lakini kwa bahati mbaya alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu.
maiti ya mtoto (5)“Tulichukua maiti, tukarejea nyumbani. Tulipofika na kuifunua tukaiona inatoka jasho kali hivyo tukaimwagia maji bakuli mbili.
“Wote tuliogopa tukakimbia, tuliporejea ndani, akatokea paka mkubwa mwenye rangi nyeusi, tukakimbia tena, akaja bibi mmoja hatumfahamu akamfukuza.”
maiti ya mtoto (7)Bibi huyo alisema kuwa, baada ya kuona hali hiyo, yeye na wanawake wenzake walibeba jukumu la kuiosha maiti hiyo ambapo wakati wanamnyoosha mkono wa kulia, marehemu huyo alipiga kelele za mtoto anayelia akilalamika maumivu, jambo lililoibua hofu kubwa hivyo watu wakakimbia.
“Tukio lingine ilikuwa usiku, tulipoifungua maiti tulikuta panya wamekula macho na masikio.
“Baada ya msururu wa mauzauza, wazazi wa marehemu waliwaita mashehe waliosoma dua ndipo hali ikatulia na muda huu tunakwenda kuzika,” alimalizia bibi huyo huku akiangua kilio.
maiti ya mtoto (6) 
Baba wa marehemu, Fikiri Mrisho
BABA WA MAREHEMU
Kwa upande wake baba wa marehemu, Fikiri Mrisho alipohojiwa na Wikienda alisema: “Inaniuma sana kwani licha ya kumpoteza mwanangu bado anaendelea kuteseka kwa mambo ya kishirikina. Hebu fikiria mwili wake kuliwa na panya! Haya ni mambo ya kutisha.”
maiti ya mtoto (8) 
NENO LA MWENYEKITI
Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Melela, Yusuf Ally Nguwa alipotakiwa kuzungumzia tukio hilo alikiri kutokea na kusema serikali haiamini mambo ya kishirikina.
Mtoto huyo alizikwa kijijini hapo huku wengi wakidai mambo hayo ni kawaida kwa Waluguru japokuwa katika tukio hilo hali hiyo ilipitiliza.

Friday, 1 July 2016

Wema Sepetu Afungukia Ugomvi Wake na Aunt Ezekiel

STAA wa filamu Bongo, Wema Sepetu amefungukia ugomvi ambao hutokea mara kwa mara na shosti wake ambaye pia ni muigizaji, Aunt Ezekiel usiingiliwe na mtu kwani wanapogombana tofauti zao wanazimaliza wenyewe na si mtu mwingine yeyote.

Akizungumza na Amani Wema alisema kuwa, yeye na Aunt ni watu waliopo karibu sana na wanaopendana hivyo inapotokea wanagombana huwa ni kitu kidogo kwao kwani huyamaliza na maisha yanaendelea kama kawaida.

“Jamani nyinyi mtuache tu, tunatibuana na Aunt, tunajuana vizuri sana ugomvi wetu ni wa mara kwa mara lakini tunamalizana wenyewe kwa sababu ukweli ni kwamba hatuwezi kukaa mbalimbali kwa muda mrefu kutokana na kupendana,” alisema Wema.

Chanzo:GPL

Kajala Aeleza Mzimu wa Kifo Unavyomtesa

Msanii maarufu wa filamu Bongo, Kajala Masanja amefunguka kuwa, maisha yake ya sasa hayajatawaliwa na furaha kwani anaona kama vile siku zake za kuishi duniani zinakaribia kuisha.
 Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni, Kajala alisema kuwa amefikia hatua ya kusema hayo kwa kuwa, kila wakati moyo wake unamuenda mbio na wakati mwingine kukumbana na ndoto mbaya zinazomfanya aogope.

“Niseme tu kwamba sina amani kwa sasa kwani nakiona kifo changu, nikilala usiku nasumbuliwa na mzimu wa kifo, nikitaka kusafiri moyo unanilipuka, nahisi itakuwa ndiyo safari yangu ya mwisho, wakati mwingine naahirisha safari kwa hofu.

“Nikiumwa kidogo tu nakosa amani kabisa, naona kama vile sitapona kikubwa namuomba Mungu aniondolee hali hii ndiyo maana nimekuwa mtu wa ibada muda mwingi,” alisema Kajala.

Thursday, 30 June 2016

Ajabu: Mwanaume Afunga Ndoa na ‘Simu Yake’ Kanisani

ndoa na simu
Mwanaume mmoja aliyejitambusha kwa jina la Aaron Chervenak mwenye umri wa miaka 34 na mkazi wa Los Angeles nchini Marekani, amefanya tukio la aina yake baada ya kufunga ndoa kanisani na simu yake ya kupapasa (smartphone).
Ndoa ya simu 2
Mwanaume huyo alisafiri hadi Vegas kulisaka kanisa moja ambalo lilimkubalia kufunga ndoa na simu yake na kula kiapo kama ambavyo alipaswa kula kiapo kwa mrembo aliyeyagusa maisha yake na kuamua kumfanya mkewe wa maisha.
Akizungumzia sababu zilizopelekea yeye kufanya tukio hilo, kupitia makala maalum ya ndoa yake hiyo, Aaron alisema kuwa ameamua kufanya hivyo kwa sababu ya ukweli kwamba simu zimekuwa zikichukua nafasi kubwa ya mapenzi na uhusiano na zikifanya jukumu kubwa la kuwatuliza watu katika dunia hii.
“Kama tutakuwa wakweli, tunaunganishwa na simu katika viwango vingi vya hisia. Tunaikimbilia kututuliza, kutulaza usingizi, kuweka unafuu kwenye mawazo yetu. Na kwangu, huo ndio uhusiano nilionao na simu yangu hii,” alisema Aaron.
Ndoa ya simu 3
“Kwa mantiki hiyo, simu yangu hii imekuwa na uhusiano wa muda mrefu na mimi na ndio maana nimeamua kufunga nayo ndoa,” aliongeza.
Kuhusu jinsi alivyokubaliwa kufanya tukio hilo kanisani, alisema kuwa alijaribu kuwasiliana na uongozi wa kanisa hilo kuona kama angeruhusiwa lakini alihakikishiwa kuwa anakaribishwa kwa mikono miwili.

Share na Marafiki: 

Shilole Na Mpango Wake Wa Kutafuta Mume Kijijini.

MKALI wa Muziki wa Bongo Fleva, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ amejutia kuwapenda wanaume wa mjini kuwa ni wavivu kila sekta hivyo anajipanga kwenda kijijini kwao Igunga,Tabora kutafuta mume.
Akistorisha na Showbiz Xtra, Shilole alisema kuwa, hataki tena kujichosha akili kwa wanaume wa mjini kwa vile ni wavivu bora aende Igunga kumpata mwanaume atakayeweza kufanya kazi kutokana na vyakula asili anavyokula.
“Wanaume wa mjini wamezoea chipsi mayai, hawawezi chochote bora wa kijijini wanakula dona na wana akili za kufikiria,” alisema Shilole.
Shilole alikuwa akitoka kimapenzi na msanii wa Bongo Fleva, Nuh Mziwanda.
-GPL

Share na Marafiki: 
 
Copyright © 2014 Kali Za Wana. Designed by OddThemes