BREAKING NEWS
Showing posts with label Nay Wa Mitego. Show all posts
Showing posts with label Nay Wa Mitego. Show all posts

Wednesday, 8 June 2016

Jionee Video ya Sanamu La Freemason iliyopo Nyumbani Kwa Nay wa Mitego


Wa mitego amekua akihusishwa sana na Freemason, hii ishu haijaanza leo imeanza toka kitambo. Hii ni kuanzia alama ambazo mara nyingi amekua akizionyesha katika video zake na hata namba za gari zake 3 ambazo zimekua zikihusishwa na mambo ya Freemason.

Sasa Nay Wa Mitego kaamua kutuonyesha na sanamu iliyo sebuleni kwake ambayo bila ubishi ni sanamu ambayo hutumika kuwatambulisha Freemason. Katika video hiyo ameonekana Nay akiwa na mtoto wao huku sanamu hiyo ikiwa kama moja ya pambo sebuleni hapo. Jioneee video hiyo hapa chini... 

Saturday, 21 May 2016

Sifanyi Muziki Kwa Ajili ya Tuzo-Nay wa Mitego

Msanii wa muziki wa bongo fleva Nay wa Mitego ambaye alisumbua sana na wimbo wake 'Shika adabu yako' ambao ulifungiwa na Baraza la Sanaa (BASATA)

na sasa ameachia wimbo wake mpya 'Saka hela' amefunguka na kusema kuwa yeye hafanyi muziki ili kupata au kushinda tuzo..

Nay wa Mitego aliyasema haya alipokuwa akihojiwa kwenye kipindi cha eNEWS na kuwataka mashabiki wa muziki wake watambue kuwa yeye hafanyi muziki ili kupata tuzo au kushinda tuzo bali yeye anafanya muziki kutoa burudani, kurekebisha sehemu anapoona si sawa pamoja na kumuingizia kipato ndiyo maana siku zote huwa anajiita mwanamuziki mfanyabiashara.
"Mimi siku zote sifanyi muziki ili nipate tuzo au nishinde tuzo hata mashabiki zangu naomba mtambue kuwa mimi sifanyi muziki kwa ajili ya tuzo" alisema Nay wa Mitego.

Katika hatua nyingine Nay wa Mitego anadai kuwa anapotoa ngoma zake za kuchana watu au kurekebisha baadhi ya mambo kwa watu au jamii huwa zinapokelewa vizuri zaidi na kuleta changamoto kwenye muziki ikiwa pamoja na kuchangamsha muziki wa bongo.

Friday, 20 May 2016

Nay wa Mitego: Gigy Money Anatafuta Kiki Kwangu

MKALI wa Ngoma ya Saka Hela, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ ameamua kumfungukia muuza nyago kwenye video za Kibongo, Gift Stanford ‘Gigy Money’ kuwa anatafuta kiki kutumia jina lake katika mahojiano anayofanya na vyombo mbalimbali vya habari.

Akichonga na Showbiz Xtra, Nay alisema kuwa amekuwa akisikia juu ya Gigy akimsema si chochote kwake na kwamba ni mbahili alishawahi kumlipa elfu ishirini baada ya kumaliza kutengeneza video zake.


 “Yaani huyo Gigy anatafuta kiki, namshangaa sana kila sehemu kunisema hovyo, kwanza hatuendani kwa chochote,” alisema Nay.

Hivi karibuni katika mahojiano na Global TV Online, Gigy alisikika akimponda Nay kuwa ni mtu bahili na haitakuja kutokea yupo naye iwe kikazi ama vyovyote kwa kuwa hana hadhi ya kuwa naye.
 
Copyright © 2014 Kali Za Wana. Designed by OddThemes