BREAKING NEWS
Showing posts with label Wema Sepetu. Show all posts
Showing posts with label Wema Sepetu. Show all posts

Tuesday, 19 July 2016

Mtoto wangu wa kike ataitwa Karma – Wema


wema

Malkia wa filamu Wema Sepetu bado hajakata tamaa kuhusu kupata mtoto licha ya kukatishwa tamaa na baadhi ya watu katika mitandao ya kijamii kutokana na uzazi wake kuwa mgumu.

Muigizaji huyo ambaye alianzisha mfumo wa APP na SMS ambao unatoa taarifa zake mbalimbali kwa mashabiki juu ya maisha yake, tayari umeanza kutoa taarifa mbalimbali kuhusu maisha yake.
Kupitia mfumo huo, Wema amesema angependa mwanae wakiume ampatie jina la Karma.
“Mtoto wangu wa kiume ataitwa Karma,” alisema Wema. “Bado sijafikiria jina nitakalo mpa mtoto wangu wa kiume japo namtaka sana mtoto wa kwanza awe wa kiume, Mungu anajua,” alisema Wema.
Pia kupitia system hiyo, Wema amewashukuru mastaa wenzake wa filamu ambao walimsupport katika show yake ya ‘The Black Tie’.

Saturday, 2 July 2016

Wema Sepetu ‘Mimi Dhahabu Inayogombewa na Watu, Sijali Wanaonichafua’


WemaSepetu

Mrembo wa filamu Tanzania, Wema Sepetu, amesema yeye ni dhahabu inayogombewa na watu hivyo hajali hata kama atachafuliwa namna gani katika mitandao ya kijamii.
Wema aliliambia MTANZANIA kwamba, hana mpango wa kujibu vibaya vinavyoongelewa kuhusu yeye kwa kuwa yeye bado ni dhahabu inayotamaniwa kushikwa na kila mtu.
“Mimi ni kama dhahabu hivyo kila mtu anatamani kuishika, watu wanaacha kufanya yao kila siku Wema, kwa sasa niko na mambo yangu ya kutafuta fedha sina habari na mtu hata aniandike vibaya vipi,” alisema Wema.
Aliongeza kwamba licha ya kusemwa, amezidi kujiongezea mashabiki na mikataba mbalimbali ya kufanya kazi na makampuni yenye majina makubwa kwa kuwa yeye ni kama dhahabu isiyochafuka.

Share na Marafiki: 

Friday, 1 July 2016

Wema Sepetu Afungukia Ugomvi Wake na Aunt Ezekiel

STAA wa filamu Bongo, Wema Sepetu amefungukia ugomvi ambao hutokea mara kwa mara na shosti wake ambaye pia ni muigizaji, Aunt Ezekiel usiingiliwe na mtu kwani wanapogombana tofauti zao wanazimaliza wenyewe na si mtu mwingine yeyote.

Akizungumza na Amani Wema alisema kuwa, yeye na Aunt ni watu waliopo karibu sana na wanaopendana hivyo inapotokea wanagombana huwa ni kitu kidogo kwao kwani huyamaliza na maisha yanaendelea kama kawaida.

“Jamani nyinyi mtuache tu, tunatibuana na Aunt, tunajuana vizuri sana ugomvi wetu ni wa mara kwa mara lakini tunamalizana wenyewe kwa sababu ukweli ni kwamba hatuwezi kukaa mbalimbali kwa muda mrefu kutokana na kupendana,” alisema Wema.

Chanzo:GPL

Wednesday, 15 June 2016

Idris Asema Wema Kutumia Tsh Milioni 4.8 kwa Ajili ya Nywele kwa Mwezi ni Hadhi yake

Baada ya mashabiki na wadau mbalimbali kujadili kauli ya Wema Sepetu ya kwamba anatumia Tsh 4.8 kwa ajili ya nywele zake kwa mwezi mmoja, mpenzi wake Idris Sultan amesema matumizi hayo yanaendana na hadhi ya mrembo huyo.

Aidha katika kauli nyingine ambayo Wema aliitoa mapema mwaka huu, alisema anatumia Sh 30,000 kwa ajili ya chakula kwa siku na kama atanunua na chakula cha mbwa wake huwa anatumia Sh 50,000 kwa siku.

Akiongea na Bongo5 wiki hii, Idris Sultan ambaye ni mshindi wa shindano la Big Brother 2014, amesema haoni tatizo kwa mpenzi wake huyo kuwa namataumizi makubwa kwa kuwa yeye mwenyewe ni mtafutaji.

“Kwa level yake anafaa, kila mtu na level yake,” alisema Idris. “Kwa hiyo nina maanisha kila mtu ana thamani yake, na kila siku hadhi ya maisha yake inapanda na pia anafanya kazi ndiyo maana anafikia katika level hiyo,”

Pia Idris alisema watu wanatakiwa kutambua kwamba jinsi uchumi wa mtu binafsi unavyokuwa basi pia na maisha yake hudabilika pamoja na muonekano.

Sunday, 5 June 2016

Diamond Platnumz Afunguka Kuhusu Wema Sepetu

Akiwa kwenye kipindi cha Friday Night Live cha EATV, Diamond Platnuzm amesema kitendo alichofanya Wema kupost kazi zake anadhani imefika wakati labda Wema Sepetu ameona hakuna sababu yeye kuendelea kumchukua Diamond Platnumz na ndiyo maana ameonyesha upendo kwa kusupport kazi zake na za wasanii kutoka kwenye Label yake.


“Kuna wakati inafika watu mnakuwa mmekuwa labda, mtu anaona hana sababu ya kuendelea kukuchukia au kuwa na vita na wewe, sababu mwanzo mwanzo mkiwa bado mnaenda mnaona kuna vitu mko navyo ndiyo maana kuna kuwa na chuki kubwa, lakini ikifika wakati kila mtu amesonga mbele na maisha yake, ameridhika na maisha yake anaona kwanini nimuwekee vita mtu fulani hivyo nadhani labda wakati huo ndiyo huu maana mwenyewe nimeona kweli amepost BET, amepost promo ya Rich Mavoko kwangu mimi nafurahi kwa sababu naona haina faida kwa sisi wasanii kuwekeana vita” alisema Diamond Platnumz

Mbali na hilo Diamond Platnumz alidai toka ameachana na Wema Sepetu hana namba yake ya simu, hajawahi hata siku moja kumpigia simu wala Wema Sepetu hajawahi kumpigia simu Diamond Platnumz.

Monday, 30 May 2016

Maneno Ya kumkejeli Wema Sepetu Yamtokea Puani Harmonize


Harmonize amelazimika kuamka na hangover ya matusi kutoka kwa mashabiki wa Wema Sepetu baada ya kusambaa video inayomuonesha akiwa na washkaji zake akishuka mistari ya hip hop inayoishia kumkejeli ex wa bosi wake, Sepetunga.
HARM
“Nasikiaga uzuri wa nyumba usikufanye utembee peku, sista duu usitoe mimba kesho ulie kama Wema Sepetu,” anaonekana Harmonize akirap na kushangiliwa na washkaji zake. Video hiyo imesababisha hasira kubwa kwa mashabiki wa Wema waliomporomoshea matusi usiku kucha kuanzia jana.
Wema aliupata ujumbe huo na aliamua kuujibu kwa busara zaidi kwa kuweka nukuu ya Angelina Jolie kwenye picha hiyo chini na kuandika tu: Well. Arent you??”
13151360_1072023689554363_894032107_n
Mpenzi wake Idris alijibu pia lakini kama kawaida kwa utani mwingi.
“As i sit here nikakumbuka kitu “Jamani nimeanzisha format yenye ustaarabu na taratibu, kwa yoyote anayetamani kutafuta kiki kupitia mimi kuna contract nimeandaa ni makubaliano mimi na wewe kwa percent ya mapato utakayopata kwa kiki hiyo ili itunufaishe wote tena ntakupa hadi na idea za jinsi ya kunitukana na kunimaliza kwasababu najua mwisho wa siku tunavuta mpunga wetu wanashangaa kesho mi na wewe tunacheka tu” hii naiita #MoneyKick #KikiPesa clients wote email me bei ni maelewano,” aliandika.
Katika kujaribu kuliua soo, Harmonize alijirekodi voice note na kuituma kwa makundi ya WhatsApp ya WCB lakini snitch mmoja aliivujisha na kuiweka Instagram. Kwenye sauti hiyo Harmonize anasikika anasema kuwa siku wanarekodi video hiyo aliomba isisambae kwakuwa aliamini ingekuja kumletea matatizo.
“Bahati mbaya imetokea hatujui nani amevujisha video imeleak,” anasema. Anadai kuwa mkakati waliojadili kufanya ni kuipigia promo ngoma mpya ya Raymond ‘Natafuta Kiki’ ili kumaliza nguvu ya video hiyo.
Kitu anachotakiwa kukifahamu Harmonize sasa ni kuwa kile kinachojadiliwa kwenye magroup ya WhatsApp ya WCB hakibaki humo tu, kuna snitches kibao wanaoweza kuumwaga mchele kwa ndege wengi hasa wasiohusika!

Hatimaye Wema Sepetu Akubali Kuolewa Na Idris, Afunguka Zaidi Hapa....!

Penzi la Wema na Idriss kwa sasa linazidi kupamba moto, mpaka kupelekea Wema Sepetu kuanza kuwaza kufunga ndoa na Idriss. Wema alifunguka hayo katika video alipoulizwa na shabiki yake ni lini atafunga ndoa na Idriss.

Tuesday, 24 May 2016

Harmonize Atoa Maneno Ya Kejeli Kwa Wema Sepetu, Bifu Zito Latabiriwa..... Angalia Video Nzima Hapa....

 
Copyright © 2014 Kali Za Wana. Designed by OddThemes