BREAKING NEWS

Thursday 30 June 2016

Rasmi: Zlatan Ibrahimovic ataja timu atakayoichezea msimu ujao

Aliyekuwa mchezaji wa timu ya PSG, Zlatan Ibrahimovic ametangaza rasmi kuwa ataichezea timu ya Manchester United kwa msimu ujao utakaoanza Agosti 13 mwaka huu.
Kadabra
Ibrahimovic ambaye alikuwa akiwaniwa na United kwa muda mrefu tangu alipomaliza mkataba wake na PSG sasa atakuwa ni mchezaji wa pili kusajiliwa na Jose Mourinho baada ya beki wa Ivory Coast, Eric Bertrand Bailly kutoka Villarreal kusajiliwa mapema mwezi huu.
Aidha Ibrahimovic (34) atasajiliwa kama mchezaji huru na Manchester United huku akitarajiwa kusaini mkataba wa mwaka mmoja kuichezea timu hiyo.

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Kali Za Wana. Designed by OddThemes