BREAKING NEWS
Showing posts with label News. Show all posts
Showing posts with label News. Show all posts

Tuesday, 19 July 2016

Mapya Mtanzania Aliyewekwa Rehani Kwa Madawa Pakistan.

NI mateso. Ndivyo unavyoweza kusema, hasa baada ya kundi la maharamia linalojishughulisha na bishara ya ‘unga’ nchini Pakistan kuelezwa kumtesa kijana Mtanzania, Adamu Akida.

Kutokana na hali hiyo, timu ya MTANZANIA ilipiga kambi jana katika eneo la Magomeni, Mtaa wa Idrissa, ambako pamoja na mambo mengine, ilifanikiwa kuzungumza na kaka wa Adamu aliyejitambulisha kwa jina la Hemed Abdallah (si jina lake halisi).

Akisimulia mkasa huo, alisema miezi minane iliyopita, Adamu alikwenda kwa kaka yake ambaye ni mtoto wa mama yake mdogo aliyetambulika kwa jina la Juma, na kuomba msaada wa mtaji kwani kazi yake ya kinyozi haikuwa ikilipa na hali ya maisha ilikuwa ngumu.

Baada ya kueleza shida yake hiyo, kaka yake huyo (Juma) alimuhoji kama yupo tayari kwa ajili ya kutafuta maisha nje ya nchi, na Adamu alikubali kufanya kazi ya aina yoyote ili mradi aweze kupata pesa.

“Adamu kwa sasa ameshikiliwa kwa muda wa miezi minane, hatujui kama alikuwa ameingia katika janga hili hadi pale tulipoona video zake katika mitandao ya kijamii. Hapa aliyepo ni baba yake mdogo, Kessy Baharia na baba yake mzazi yupo Bagamoyo Mlingotini, ndiko anakoendelea na maisha yake.

“Awali alikwenda kwa kaka yake mtoto wa mama yake mdogo anaitwa Juma na kuomba asaidiwe mtaji kwani amekuwa na maisha magumu sana. Baada ya hali hiyo aliambiwa kuna safari ya kwenda Pakistan ambayo waliondoka wakiwa wameambatana watu watatu pamoja na Juma na kijana mwengine ambaye jina lake limenitoka, ila anaishi Kinondoni.

“Walipofika kule, Juma akachukua mzigo akiwa na yule kijana wa Kinondoni, huku Adamu akiachwa Pakistan kwa maelezo kuwa baada ya siku tano atakuja nchini na mzigo mwingine. Muda wote hata tukihoji alipo Adamu tunaambiwa yupo anaendelea na kazi huko aliko ana angerudi mwezi wa tisa nane.

“Sasa hii video ndiyo imetupa picha halisi ya Adamu, maskini sijui kama tutampata akiwa hai. Hata hivyo kwa kipindi cha hivi karibuni, tulikuwa tukishangazwa na mwenendo wa Juma kwani amekuwa na fedha nyingi sana hadi kufikia kuwajengea nyumba dada zake pamoja na kuwanunulia magari,” alisema Abdallah huku akibubujikwa na machozi.

Mke wake

Inaelezwa kuwa mke wa Adamu ambaye alikuwa akiishi Mtaa wa Sunna, Magomeni, alihamia Kijitonyama.

Kwamba alihamishwa na shemeji yake, Juma ambaye ndiye aliyempangia nyumba nyingine Kijitonyama.

“Katika suala hilo, tuna shaka kuwa hata mke wa Adamu anajua kinachoendelea, maana miezi mitatu iliyopita alihama Magomeni na kuhamia Kijitonyama, tena huku akisema mume wake karibu anarejea nchini.

“Lakini baada ya video kuanza kuonekana, sasa hata kupatikana hapatikani, na hatujui amehamia nyumba gani huko Kijitonyama,” alisema Abdallah.

Serikali ya Mtaa

Akizungumza na MTANZANIA, Mwenyekiti wa Srikali ya Mtaa wa Idrissa, Issa Mpangile, alisema kuwa jana askari kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi walifika katika ofisi yake na kumtaka waongozane kwenda katika nyumba ya baba mdogo wa Adamu.

Alisema walipofika nyumbani kwa Kessy Baharia, ambaye ndiye baba mdogo wa Adamu, polisi walichukua maelezo yake na baadaye wakarudi katika ofisi ya Serikali ya Mtaa kuchukua maelezo ya mwenyekiti huyo.

Akizungumza kuhusu kijana huyo, Mpangile alisema kuwa ni mzaliwa wa mtaa huo, lakini baadaye alihamia Mtaa wa Suna ambao ni jirani na Mtaa wa Idrissa, Kata ya Magomeni.

Alisema wakati kijana huyo anahama mtaa huo, alikuwa bado ni kinyozi na hakuwa na rekodi ya kusafiri kwenda nje ya nchi.

“Wakati Adamu anahama Mtaa wa Idrissa, alikuwa bado ni kinyozi na hakuna rekodi kwamba alikuwa anasafiri nje ya nchi,” alisema Mpangile.

Alisema katika mazungumzo na Baharia, alimweleza kuwa amewasiliana na baba wa kijana huyo ambaye anaishi Bagamoyo mkoani Pwani.

Mpangile alisema kwa mujibu wa Baharia, baba wa kijana huyo anayejulikana kwa jina la Akida, amesikia habari za mtoto wake na kwamba atakwenda kuripoti kituo cha polisi.

Naye mama mdogo wa Adamu, aliyetambulika kwa jina la Khadija Katundu, alikiri maofisa wa polisi kumuhoji mume wake.

Alisema wameendelea kutoa ushirikiano kwa watu wanaofika nyumbani kuhoji kuhusu suala hilo, na kwamba wanaamini ufumbuzi utapatikana.

Serikali yahaha

Baada ya taarifa hizo kuripotiwa na gazeti hili jana, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia Jeshi la Polisi wanafanya mawasiliano na Serikali ya Pakistan ili kuangalia namna ya kumwokoa Adamu katika mikono ya maharamia hao.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Msemaji wa Polisi, Advera Bulimba, alisema tayari wamepata taarifa dhidi ya Mtanzania huyo.

“Kwa sasa tunafanya mawasiliano na wenzetu wa Pakistan tuone namna ya kumtoa kijana huyo katika mikono ya hao watekaji, na tukikamilisha hilo tutatoa taarifa rasmi juu ya jambo hili,” alisema Advera.

Wakati hayo yakiendelea, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, kupitia mmoja wa maofisa wa idara ya habari ambaye hakupenda kutajwa jina lake gazetini, alisema wamepata taarifa ya tukio hilo, na sasa wanafanya mawasiliano na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Source: Mtanzania

Monday, 18 July 2016

Makonda Akanusha Wasio Na Kazi Kukamatwa







Kumekuwepo na taarifa ambazo zimekuwa zikisambaa na zimekuwa zikimnukuu Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda kuwa ametoa agizo la kufanyika ukaguzi kwa kila nyumba na ambao watakutwa hawana shughuli maalum basi wakamatwAAkizungumza katika kipindi cha Power Breakfast kinachoruka kupitia Clouds Fm, Makonda amekanusha taarifa hizo na kusema kuwa jambo hilo halina ukweli wowote na kinachofanyika ni baadhi ya watu kusambaza taarifa hizo katika mitandao ya kijamii.
“Sasa tuwakamate wote tunawapeleka kwenye magereza gani?, hilo jambo halipo hivyo, sisi tunataka kuwafahamu watu wetu ili hata linapokuja jambo la maendeleo tujue tunaenda kuwapa watu sahihi,
“Mfano kwa sasa tuna mpango wa kuchukua vijana 1,200 tuwapeleke katika mafunzo ya ufundi na ujasiriamali kwa miezi mitatu sasa kama hatuwatambui tutawapa nafasi watu wengine ambao sio wa Dar lakini tukiwafahamu inakuwa rahisi,” alisem Makonda.
Aidha Makonda amekanusha kuwa na akaunti katika mitandao ya kijamii ambazo zinaanza na neno la RC au DC hivyo kuwataka watumiaji wa mitandao kuwa makini na watu hao.
“Mimi JamiiForum, Facebook na Instagram natumia jina moja la Paul Makonda sina jina tofauti na hilo,” alisema.

Saturday, 2 July 2016

RC Makonda Atangaza Vita Kwa Mashoga waliopo jijini Dar es Salaam

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ametangaza vita na makaka poa (mashoga) na madada poa (makahaba) walioko jijini Dar es Salaam kuwa utaendeshwa msako mkali wa kuwaondoa.

Mkuu wa Mkoa huyo aliyasema hayo kufuatia hali ya vitendo hivyo visiyokubalika na jamii kuzidi kushamiri na kuwa kuna hatari kubwa ya watoto wadogo kuiga vitendo hivyo vinavyoleta picha mbaya kwani ni kinyume na maadili ya mtanzania.

Aidha alisema hawezi kuifumbia macho hali hii kwani inamomonyoa maadali ya jamii na kuwa yuko tayari kulivalia njuga suala hili ili kuhakikisha anawamaliza wote mkoani

Sakati hili la ushoga na ukahaba limeibuka siku za hivi karibuni baada ya kituo cha televisheni cha Clouds Tv kumhoji shoga mmoja ambapo jamii ilipinga kitendo hicho na kuona kama walikuwa wakiuhalalisha ushoga na kuaminisha jamii kuwa ni kitu kizuri.

Friday, 1 July 2016

Ni Kosa Kubwa Sana Kumfananisha Rais Magufuli na Dikteta

Kuna mawili, either watu hawajui maana na dhana nzima ya udikteta ama kwa makusudi wameamua kupotosha jamii. Viongozi mbalimbali hasa wa upinzani wamesikika wakimwita Magufuli kama Rais dikteta. sio kweli hata kidogo..

Nini Maana ya Dikteta?, Dikteta ni aina ya utawala wenye kutoa amri kama Imla. Ni neno la kumtaja mtawala asiyebanwa na sheria na hutumia nguvu ya dola kuendeleza utawala wake na kutokubali upinzani.... Kama Magufuli asingekubali upinzani si angefuta vyama vya siasa?. Ni marangapi kapokea mawazo wa wapinzani? (rejea alivyotembelewa na Maalim Seif na Prof. Lipumba ambao ni wapinzani)..

Sifa Kuu za Dikteta...
1, Mtu anayeshika mamlaka yote mikononi mwake.... Tokea lini Rais kashika mamlaka yote mikononi, je mawaziri wanaotumbua, wakuu wa mikoa wanaotumbua, wakuu wa wilaya wanaotumbua, PM anavyotumbua ushasikia wameingiliwa na Rais?... Mnyonge mnyongeni ila haki yake apewe. Magufuli yupo kwa ajili ya sisi wanyonge...

2. Hakubali Uchaguzi wa kisiasa au anahakikisha uchaguzi si huru...Magufuli huyu alibariki uchaguzi wa meya wa Dar es Salaam kufanyika na Ukawa wakashinda, angekuwa dikteta angebariki au kukubali uchaguzi huo?. Juzi na jana Ukawa walifurahi baada ya wagombea wao kushinda nafasi ya wenyeviti vya vijiji huko Geita, mbona huyo mnayemwita dikteta kakubali matokea?.....

3. Haheshimu haki za binadamu...... Hii ni moja ya sifa ya Rais dikteta... Wananchi tunashangaa kuona wapinzani wanamwita Magufuli ni dikteta. ni wazi hakuna mtu anayeheshimu haki za binadamu hasa wanyonge kama Rais Magufuli. kila speech anayotoa ni kulilia wanyonge, kila tukio anapoenda Magufuli ulilia wanyonge sasa kama haheshimu haki za binadamu angelilia wanyonge?

4. Anatoa amri kama sheria... Ni lini Rais Magufuli katoa amri bila kufata sheria?. Mara zote Magufuli amekuwa akifanya maamuzi kwa kufata katiba, sheria zilizopo nchini..... na sheria (bill) wabunge ndio walizitunga ambapo ndani ya bunge wapo wabunge wa upinzani... Tuacheni Rais Magufuli apige kazi..

5. Bunge na mahakama kufata maagizo yake..... Moja ya jambo tunalolivunia kama taifa ni uhuru wa bunge na uhuru wa mahakama. kama bunge lingekuwa linafata maagizo yake mbona inatokea kipindi wapinzani wanashinda kwa hoja (rejea 5 years Plan, ambapo Mwanasheria Mkuu alichemsha). Bunge hili limeonyesha liko huru, tena sana. kinachotokea ni ukomavu na ushupavu wa Dr. Tulia kama kiongozi wa bunge... Mahakama pia ziko huru, na ndio maana tumeona hata wapinzani wakishinda katika kesi mbalimbali za uchaguzi zinazowakumba... na hata kitendo cha wapinzani kukimbilia mahakamani pale wanapobanwa ni kiashiria tosha kuwa mahakama ni huru na Rais au serikali haiingilii mahakama...

NB: Hivyo ni kosa kubwa sana, tena sana kumlinganisha, kumfananisha au hata kujaribu kumfananisha Rais Magufuli na watu kama Adolf Hitler, Benito Mussolin, Mao Zedong, Augusto Pinochet, Pol Pot, Idi Amin au Sani Abacha.......

Magufuli kaamua kwa dhati kabisa kutumikia wanyonge. kaamua kwa dhati kabisa kuwa mzalendo kwa kuwapigania na kupigania haki za wanyonge. hivyo tumuache apige kazi... tusubiri 2020 muda wa siasa....

Imeandikwa na Pagan Amum/JF

Friday, 17 June 2016

Exclusive: Ripoti ya redio na TV za Tanzania zenye watazamaji/wasikilizaji wengi zaidi

Kituo cha ITV kinachomilikiwa na kampuni ya IPP Media Group kwa mara nyingine tena kimeongoza kwa kuwa na watazamaji wengi zaidi miongoni mwa vituo vya runinga nchini.
Radio Tanzania
Kwa mujibu wa data za robo ya mwisho ya mwaka 2015 na robo ya kwanza ya mwaka 2016 kutoka kwenye kampuni ya utafiti wa vyombo vya habari Geo Poll yenye makao yake nchini Marekani, kituo hicho kilichukua asilimia 20 ya watazamaji (audience share) katika miezi minne ya mwisho (October – December) ya mwaka 2015 na kushuka kwa 2% katika kipindi cha miezi minne ya kwanza ya mwaka 2016 (January – April), kwa kuwa na asilimia 18.
GTV1
Clouds TV imeendelea kufanya vizuri pia kwa kukamata nafasi ya pili kwa kuwa na 17% katika robo ya nne ya mwaka jana huku ikipanda kwa 2% katika robo ya kwanza mwaka 2016 hadi kufikisha 19%.
Ripoti hiyo imeonesha pia kuwa EATV imefanya vizuri katika robo ya kwanza mwaka huu kwa kuwa na 16%.
Vituo vilivyofuata ni pamoja na TBC 1, Star TV, Channel 10, TV1, TBC 2. Vingine vikiwemo Azam TV, Mlimani TV, Capital TV na vingine vimeonekana kufanya vibaya kwa kugawana 1% tu iliyosalia, kwa mujibu wa ripoti hiyo.
GTV2
Kwa upande wa ratings, East Africa TV na TV1 ziliongeza katika robo ya kwanza huku ITV ikipoteza ratings kwa kiwango kikubwa. “TBC1 and Channel 10 have also dropped in their ratings in Q1,” inasema ripoti hiyo.
RADIO
Kwa upande wa vituo vya redio, Clouds FM bado imeendelea kuwa kinara kwa kuvuta 28% ya wasikilizaji katika robo ya mwisho 2015 huku ikipoteza 2% katika robo ya kwanza mwaka huu na kuwa na 26%.
GT Radio 1
TBC Taifa imeonesha kufanya vizuri kwenye robo ya kwanza mwaka huu kwa kuwa na 13% ikifuatiwa na Radio Free Africa iliyong’ang’ania kwenye 10% huku Radio One na TBC FM zikifuatia. Habari njema kwa EFM ambayo hadi sasa bado inasikika Dar es Salaam na Pwani pekee ambayo imeendelea kufanya vizuri kwa kuwa na wastanii wa 5.5% mbele ya East Africa Radio, Times FM na Capital FM.
GT Radio 2

Jiunge na Bongo5.com sasa

Saturday, 21 May 2016

Yajue Madhara Watakayoyapata Wajawazito Kwa Kula Chipsi....

Kila siku asubuhi huwa nazisogeza headlines zilizobebwa kwenye kurasa za Magazeti ya Tanzania, Uchambuzi wa stori zote napandisha kwenye account yangu ya Twitter >>>@millardayo.
Tayari nimezikusanya stori za Magazeti ya May 21 2016 na waweza kuzipitia hapa chini moja baada ya nyingine, moja ya stori kubwa ni hii kauli ya mtaalamu wa lishe wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Denis Mbinga katika mahojiano na Gazeti la Mtanzania.
Katika mahojiano hayo Mbinga alisema matatizo ya watoto kuzaliwa na vichwa vikubwa , mgongo wazi na magonjwa mengineyo katika siku za karibuni yameongezeka kutokana na ulaji wa vyakula visivyofaa na hasa chipsi na vile vilivyosindikwa viwandani.
 
Copyright © 2014 Kali Za Wana. Designed by OddThemes