BREAKING NEWS

Monday 4 July 2016

​Picha: Ommy Dimpoz, Wayne Rooney Wakila Bata Ibiza, Hispania

Kama kuna sehemu inayotembelewa zaidi duniani na watu ambao hawana kabisa stress ya kitu kinachoitwa ‘Pesa’ basi Ibiza, Hispania inaongoza.

Ibiza ni kisiwa cha raha, burudani, starehe na bata la kila aina. Ni sehemu ambayo nyota wa Manchester United na England, Wayne Rooney na familia yake wanapumzika kwa sasa baada ya timu yake ya taifa kutolewa kwenye Euro 2016.
Ommy Dimpoz ni miongoni mwa watu wanaofurahia hewa ya Ibiza kwa sasa.

Hitmaker huyo yupo kisiwani humo katika kile kinachoweza kuwa ni ‘vekesheni’ yake ya aghali zaidi kuwahi kuifanya.

Anamfanya kila mtu aone wivu kwa maisha na raha anayopitia sasa. Kucruise kwenye speed bot na kuchezea maji ya bahari ya Mediterranean.

Staa huyo amepost video akiwa kwenye boti na watu wengine wawili, msichana , Milly na nahodha wa kizungu aliye kifua wazi. Hakika Ommy katisha.

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Kali Za Wana. Designed by OddThemes