BREAKING NEWS

Thursday 30 June 2016

Shilole Na Mpango Wake Wa Kutafuta Mume Kijijini.

MKALI wa Muziki wa Bongo Fleva, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ amejutia kuwapenda wanaume wa mjini kuwa ni wavivu kila sekta hivyo anajipanga kwenda kijijini kwao Igunga,Tabora kutafuta mume.
Akistorisha na Showbiz Xtra, Shilole alisema kuwa, hataki tena kujichosha akili kwa wanaume wa mjini kwa vile ni wavivu bora aende Igunga kumpata mwanaume atakayeweza kufanya kazi kutokana na vyakula asili anavyokula.
“Wanaume wa mjini wamezoea chipsi mayai, hawawezi chochote bora wa kijijini wanakula dona na wana akili za kufikiria,” alisema Shilole.
Shilole alikuwa akitoka kimapenzi na msanii wa Bongo Fleva, Nuh Mziwanda.
-GPL

Share na Marafiki: 

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Kali Za Wana. Designed by OddThemes