BREAKING NEWS

Friday 20 May 2016

Nyota Ya Drake Yazidi Kumulika Kwenye Tuzo Za BET


drake

 Drake amezidi kuonyesha ubora wake kwenye tuzo za BET zitakazofanyika, Juni 26 huko Los Angeles, Marekani.
Mwaka 2016 umekuwa wa neema kwa Drake baada ya kuonekana mara tisa kati ya vipengele sita alivyowekwa akifuatiwa na Beyonce pamoja na Rihanna. Pia albamu yake ya ‘Views’ inazidi kushika namba moja kwenye chati za Billboard baada ya kuuza nakala zaidi ya milioni 1.04 ndani ya wiki mbili tangu alipoiachia mwishoni mwa mwezi Aprili.
Tuzo hizo za BET zitafanyika kwenye ukumbi wa Microsoft Theater, Los Angeles huku Afrika Mashariki tukiwakilishwa na Diamond kwenye kipengele cha Best International Act: Africa lakini pia atafanikiwa kufanya show kwenye tuzo hizo.

 Bongo5.com

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Kali Za Wana. Designed by OddThemes