BREAKING NEWS

Tuesday 24 May 2016

Lady Jaydee Haikufaa Uimbe Uliyoimba Ndani ya Wimbo wa Ndindindi

Nijikite Madani.

Bila Shaka watu wengi humu tuna mkubali sana mwanamziki Huyu nguli wa miondoko ya r n b ndani ya bongofleva. Huyu Ni kati ya wasanii wakubwa waliofungua uhusiano mzuri wa kimziki baina ya Tanzania Na Afrika kusini ref; Njalo! Hata kuna video Jide aliwahi kufanya Kule bondeni, kufuatia harakati zake Leo hii wasanii wengi wakubwa wanaowika Miaka hii wanafuata Nyayo zake Na kujaribu kupanua wigo wao wa mashabiki barani Africa Na duniani Kwa ujumla kupitia mlango uliofunguliwa Na Jide huko SA.

Wote tunafahamu mahusiano Na Ndoa aliyopitia dada yetu Huyu kipenzi. Tunajua changamoto kubwa aliyokabili katika Ndoa Yake ambayo Kwa kiasi kikubwa ilikua inampact KUBWA tu kimafanikio Yake ya kimziki .

Ni Kweli huenda Shemeji yetu (G) amemkosea Mara nyingi dada yetu Ila Kwa maoni yangu Mimi bado Naona alikua Na mchango Mkubwa sana Kwa dada yetu( sijasema Jide hawezi kusimama kimziki bila G) Ila nafikiri haikua vema kumuimba mtaliki wake katika wimbo huo!

Ikumbukwe G alivumilia maneno mengi sana kuhusu hali ya Huyu dada yetu! Hata zaidi G mwenyewe sio mtu wa visasi Na majibizano! Amekua cool sana kuzungumzia mahusiano Na hali Yao ya mahusiano Yaani Kwa kifupi Jamaa ameonyesha Kifua cha kiume Na Heshima Kwa aliekua mkewake.

Jide anamashabiki wengi sana, Yaani hata angeimba chochote bado ngoma Yake Ingelizwa sana tu! Hata angetaka kuimba kipaji chake Kua kimejaa Ndindindi bado ingefaa tu. Ukiangalia umri wake Na jinsi amejijengea heshima Kwa mashabiki Na maadui zake ilifaa aonyeshe ukomavu Kwa ku'move on bila kuzungumzia lolote kuhusu Ndoa vunjifu!

Mwisho Kabisa ili tuendelee kukuheshimu Kama Sasa dada yetu kipenzi Tunaomba usizungumze lolote kuhusu G, wewe simama kivyako tu, sote tunajua uliyopitia ingawa kiundani zaidi unajua mwenyewe, Na huenda unaimba Ili kupunguza machungu Ila jikaze, kumbuka wewe Ni Komando! Muache brother aendelee tu Na Maisha Yake, Hebu ona hata Hakumzuia Dina kufanya interview Na wewe ingawa Na uhakika angetaka angezuia tu!

IMBA TUCHEZE!!

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Kali Za Wana. Designed by OddThemes